Psalms 107:1-6

(Zaburi 107–150)

Kumsifu Mungu Kwa Wema Wake


1 aMshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema,
upendo wake wadumu milele.

2 bWaliokombolewa wa Bwana na waseme hivi,
wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,

3 cwale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali,
kutoka mashariki na magharibi,
kutoka kaskazini na kusini.


4 dBaadhi yao walitangatanga jangwani,
hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.

5 eWalikuwa na njaa na kiu,
nafsi zao zikadhoofika.

6 fNdipo walipomlilia Bwana katika shida yao,
naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Copyright information for SwhKC