Psalms 107:1-6
(Zaburi 107–150)
Kumsifu Mungu Kwa Wema Wake
1 aMshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema,
upendo wake wadumu milele.
2 bWaliokombolewa wa Bwana na waseme hivi,
wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 cwale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali,
kutoka mashariki na magharibi,
kutoka kaskazini na kusini.
4 dBaadhi yao walitangatanga jangwani,
hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 eWalikuwa na njaa na kiu,
nafsi zao zikadhoofika.
6 fNdipo walipomlilia Bwana katika shida yao,
naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Copyright information for
SwhKC